Kabla sijazungumzia tiba ya tezi dume napenda kwa ufahamu japo kwa ufupi tezi dume ni nini? Maana wengi wetu tukisikia neno hilo huwa tunafikiria ni ugonjwa kitu ambacho sio ukweli hata kidogo.
Ukisikia tezi dume naomba ufahamu kuwa ni kiungo kwenye mwili wa mwanaume kinachofanya kazi ya kutengeneza shahawa (yale maji maji ambayo mwanaume huwa anayatoa anaposhiriki tendo la ndoa). Ndani ya yale maji ndio huwa kuna mbegu za kiume ambazo huwa zinaitwa manii (Sperms). Hivyo ni kiungo chenye kazi ya muhimu kabisa kwa mwanaume, sasa nafikiri utapenda kufahamu inakuwaje linakuja tatizo la tezi dume, ni pale ambapo kiungo hiki huwa kinavimba na kuna wakati kikishavimba ndio kansa huanza kujenga kwenye huo uvimbe ndipo hapo kansa ya tezi dume inapokuwa. Hiyvo naomba ufahamu kuwa kuvimba kwa tezi dume na kansa ya tezi dume ni vitu viwili tofauti japo vyote viwili vinaweza kutibiwa na dawa hii ntakayokuelekeza leo. Lakini napenda ufahamu mara nyingi tatizo hili la kuvimba kwa tezi dume hutokea ikiwa mwanaume unakuwa mvivu kushiriki tendo la ndoa mara kwa mara. Kikawaida mwanaume unatakiwa kupiga angalau bao 21 kwa mwezi ili uwe na afya nje, sasa ukiweza mzembe ndio unakaribisha tatizo hili la tezi dume. Twende kwenye matibabu yake.
Mahitaji:
Majani ya mstafeli au unga wa majani hayo
Matayarisho na matumizi yake:
Chukua majani mabichi 10 au kijiko kikubwa kimoja cha unga wa majani hayo ya mstafeli na uchemshe kwenye maji nusu lita kwa dakika 7 hadi 10, epua na uache ipoe kabisa kisha chuja upate maji yake.
Mgonjwa anywe kikombe kimoja cha chai kutwa mara 2 kwa siku 30 hadi 60. Vile vile mgonjwa anatakiwa kuzingatia utaratibu wa kula kama nilivyoelekeza kwenye sura ya kwanza ya kitabu hiki. Lakini kumbuka kuwa sababu kubwa ya kwanza inapelekea tatizo hili ni uvivu wa kushiriki tendo la ndoa mara kwa mara.
Ikiwa sehemu uliyopo sio rahisi kwako kupataMajani haya ya Mstafeli basi Tafuta Kiazi Pori au kwa Kizungu kinaitwa African Wild Potatoes watu wa Kigoma wanakifahamu sana hiki kiazi pori. Chemsha kiazi hiki na unywe maji yake kutwa mara 2 kwa siku 30 hadi siku 60 kwa uwezo wa Mungu utakuwa umepona kabisa tatizo hilo la Tezi Dume.
Asante kwa elimu
Ahsante sana kwa kutumia muda wako wa thamani kusoma makala zetu