Makosa 2 Yanayofanywa na Watu Wanaopunguza Uzito

 

Kosa la 1: Kudhani “Kupungua” ni Swala la Chakula Gani unakula,

Tangu tukiwa wadogo, tumelishwa uongo kwamba ili upungue lazima uache kula vyakula vyako unavyovipenda na kuanza kula vyakula vya gharama kama mayai, maziwa, au mboga za majani pekee.

Huu ndio mtego mkubwa unaokufanya ushindwe kila siku!

Sayansi halisi ya mwili haijali sana unachokula, bali inajali kitu kikubwa zaidi ambacho kipo ndani ya miili yetu lakini kimeganda na kulala—kitu kinachoitwa Metabolism. Kila unapobadilisha ratiba yako ya milo bila kujua spidi ya Metabolism yako, unaupiga mwili wako ngumi ya uso na kuufanya uhifadhi mafuta zaidi kwenye tumbo na nyonga.

Je, unaiamshaje hii Metabolism ili ichome mafuta hata ukiwa umelala?

Kosa la 2: Kufuata “Ratiba ya Milo” ya Mazoea badala ya kufuata Alama (Signal) Rasmi ya Mwili Wako

Watu wengi wamekariri kuwa lazima ule asubuhi, mchana, na usiku. Kula kwa kufuata saa au ratiba ya ukutani ndio makosa makubwa yanayotengeneza vitambi vya ajabu.

Mwili wako una mfumo maalum wa kukuambia: Sasa hivi nina uwezo wa kuchoma chakula” na “Sasa hivi nikila nitaenda kuhifadhi kama mafuta mwilini.”

Lakini kwa sababu ya mazoea, umekuwa ukilazimisha kuweka chakula mdomoni wakati mwili wako haujatoa ile Signal rasmi. Matokeo yake?

Chakula hicho kinajigeuza kuwa mafuta au kinasababisha changamoto ya tumbo kujaa gesi au kinesi kwa sababu hakisagiwi vizuri.

Je, hiyo Signal (alama) ya mwili ni ipi, na unaitumiaje kujua muda sahihi wa kula bila kuacha kula wali au ugali wako unaoupenda?

Ukizijua siri hizi, utapungua kishua kabisa bila kuwa mtumwa wa maisha yako

Mambo haya nimeyaeleza kwa upana sana kwenye kitabu changu cha JINSI YA KUPUNGUZA UZITO KISHUA. Ndani ya kitabu hiki unakwenda kujifunza mambo mengi sana unapaswa kuyajua ili uweze kupunguza uzito kirahisi na upate matokeo ya kudumu.

Kitabu hiki ni BURE KABISA bonyeza hapo chini uweze kudownload na ujifunze mambo yote muhimu.

               DOWNLOAD KITABU CHA BURE HAPA

About the author

Topten Herbs

Topten Herbs ni kituo cha utafiti wa Tiba mbadala zinazoweza kusaidia jamii yetu kujitibia maradhi mbalimbali yanayotukabili kirahisi kabisa kwa kutumia vitu mbalimbali vinavyotuzunguka katika mazingira yetu. Kituo hiki kinapatikana Mbezi kwa Msuguri jijini Dar es Salaam.

View all posts

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *